Rekodi ya Tanzania Kwenye Siku ya Mgambo Duniani (31 July) - World Ranger Day.


Ivi unafahamu kwamba tarehe zote katika mwaka mzima huambatana na maadhimisho au sikukuu za kimataifa? Tarehe 31 Julai ni siku ya kimataifa ya wanamgambo wa hifadhi za taifa Duniani. Wanamgambo hawa wanamajukumu ya kulinda hifadhi dhidi ya ujangiri na kuzingatia maisha ya wanyama kama Tembo, Faru nk

Siku hii ya kimataifa husimamiwa na International Ranger Federation (IRF). IRF ni shirika lililoanzishwa tarehe 31 July 1992 huko nchini uingereza. Tanzania ni miongoni mwa wanachama wa IRF. 
IRF wana utaratibu wa kutoa tuzo zao kila baada muda wa miaka kadhaa.. Mnamo mwaka 2018 Mgambo kutoka Tanzania, Wayne Lotter alitunukiwa tuzo ya Lifetime Achievement Award (Tuzo ya heshima). Jina la tuzo pekee linaashiria kuna kazi ya ziada aliifanya Mgambo huyo. 

Ngoja nikujuze, Wayne Lotter alipoteza maisha yake akiwa katika harakati za kupambana na majangiri hifadhini. Sasa kwa kuzingatia uduni wa mazingira ya kufanyia kazi na vitendea kazi, IRF iliamua kumpa Mtanzania huyu tuzo ya heshima! Tanzania ndio nchi inayoshikilia rekodi hii mpaka pale tuzo zingine zitakapofanyika. 

Nimekuandikia makala hii ili kuonesha na kutambua mchango wa Wanamgambo wa hifadhi za Tanzania katika Utalii. Wakifanyia kazi zao katika mazingira hatarishi na katika upungufu wa vifaa wanaipeperusha bendera ya Tanzania katika uso wa dunia tarehe 31 July (World Ranger Day) na kuvutia watalii wengi zaidi. 

Asante kwa kusoma makala hii, bofya hapa kufamu zaidi kuhusu IRF na World Ranger Day.   

Post a Comment

0 Comments